Kalonzo atamatisha mkataba na Nasa ,ajiunga rasmi na Jubilee

Kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka  ametnagaza mipango ya kujiondoa rasmi kutoka muungano wa NASA unaoongozwa na Raila Odinga ili kujiunga na   Jubilee .

Kamati ya usimamizi wa chama cha Wiper  ilikutana kupitia njia ya mtandao na kupitisha uamuzi wa  kujiunga katika muungano na chama cha Jubilee kinachoongzowa na rais Uhuru Kenyatta .

Hatua hiyo sasa inamaanisha kwamba  iper sasa itaondoka kutoka muungano huo wa upinzani kwani sheria  hairuhusu chama kimoja kuwa katika zaidi ya muungan mmoja .

Chama cha Kalonzo pia kitalazimika kumuandikia msajili wa vyama Anne Nderitu kumfahamisha rasmi kuhusu uamuzi wa kujiondoa kutoka NASA na kuiunga na muungano mpya .

Ili muungano wa NASA kuvunjiliwa mbali kabisa vyama tanzu  vitatu vinafaa kuondoka  lakini kwa sasa ODM ,ANC na Ford Kenya bado vipo katika muungano huo .