Kutoka Papa Dennis hadi kwa Njenga Mswahili tazama Celebs wote walioaga dunia wakiwa maskini
Kifo cha msanii wa gospel Papa Dennis kimefichua jinsi wasanii wengi wanavyoteseka katika lindi la umaskini licha ya wengi kufikiri kwamba wana pesa kwa ajili ya mtindo wa maisha yao .
Hii hapa orodha ya baadhi ya wasanii na celebs taika ambao vifo vyao vilifichua jinsi hali ilikuwa ngumu kwao
- Papa Dennis
Kifo cha Papa Dennis kiliwashtua wengi baada ya mwili wake kupatikana huko Pangani . Papa alionekana kuwa a yote ikizingatiwa kwamba alitokea Gheto na kufaulu kujipata katika ulingo wa muziki .
Baadaye alifukuzwa kutoka nyumba yake aliokuwaamepangisha bada ya kukosa kulipa kodi na kisha kuanza kuihi kama skwota pangani katika studio za kurekodi muzik kabla ya kifo chake .
- Mzee Ojwang
Kwa watoto waliozaliwa miaka ya 80 na 90 hakuna asiyemjua mzee ojwang’ na jinsi alivyokuwa akiwapasua mbavu kwa vituko vvyake katika kipindi cha Vioja mahakamani .
Kwa muda mrefu alikuwa akiigiza pamoja na mama kayai . Aliaga dunia julai mwaka wa 2015 baada ya kupata maradhi ya numonia . kabla ya hapo alikuwa ametibiwa baada ya kuanza kupata matatizo ya macho na serikali ikaifutilia mbali bili ya matibabu yake katika hospitali ya KNH
- Achieng Abura
Achieng aliaga dunia oktoba mwaka wa 2016 katika hospitali ya KNH .kabla ya kifo chake alikuwa ameitisha hafla mbili za michango na watu wengi walijitokeza kutoa pesa za kumsaidia kupokea matibabu yake .
Katika mahojiano alimueleza Biko Zulu kwamba alikuwa akipata matatizo ya kupata pesa za kumpeleka mtoto wake kwa matibabu nchini Uingereza mwanae alikuwa na anemia.
Na katika hafla moja ya kuchangisha pesa chini ya watu 10 ndio waliojitokeza nan i baada ya kifo chake ndipo kila mtualitaka kutajwa pamoja na jina lake kubwa .
- Joe Kadenge
Mwanasoka stadi sana Joe Kadenge aliaga dunia katika hospitali ya Merdian ,Nairobi
Kulingana na mwanawe Oscar ,afya ya bbake haikuwa nzuri kwa muda mrefu na kwa mtu wa taadhima na sifa zake wengi walishangaa jinsi alivyotelekezwa kwani akitbiwa NHIF ililazimika kumlipia bili ya shilingi milioni 2
Kinaya ni kwamba licha ya kuhitajimsaada akiwa hai ,bajeti yake ya mazishi iligonga shilingi milioni 5.
- Njenga Mswahili
Mchekeshaji huyo wa Churchill aliaga dunia Novemba mwaka wa 2019 baada ya kugongwa na treni .
Wengi walijua kama Njenga Mswahili – jina halisi James Anthony Njenga – na mwili wake uliobabadiwa ulipatikana katika mkondo wa treni mtaani Dagoretti .
Njenga alifahamika kwa kutoa ucheshi wake katika lugha ya Kiswahili ndiposa alipewa jina hilo –mswahili .kabla ya kifo chake alikuwa amepatwa na msongo wa mawazo na kwa bahati mbaya hakitajulikana kilichomtia katika hali hiyo .