Tunahitaji pesa na msaada wa Ruto,makasisi na wahubiri wasema
Baadhii ya makasisi na wahubiri kutoka North Rift wanamunga mkono uhusiano wa karibu wa naibu wa rais na kanisa kwa sababu ya msaada wake na pesa wakisema wanazihitaji .
Wakiongozwa na Askofu Simon Kemei wamesema pesa zozote zinazopewa makanisa zimetakaswa bila kujali zilizkotoka .
Kimei siku ya jumanne amewapuuza wanaopinga hatua ya Ruto kuwa mkarimu kwa makanisa na kumtaka Ruto kuyasaidia makanisa yote yakiwemo katika eneo la North Rift .
Ruto amekuwa mkarimu kwa makanisa na viongozi wa kidini huku misaada yake pia ikiwafikia vijana na makundi ya akina mama ili kuwekeza katika miradi ya kujipata mapato
“ kama viongozi wa kidini tumefurahi sana na anachofanya naibu wa rais kuyapa misaada makanisa na tunaamini anatumiwa an Mungu kuwasaidia watu wanaohitaji msaada wake’ amesema Kemei
Alikuwa akizungumza huko Eldoret baada ya maombi ya mkutano wa maombi ya wiki nzima. Makanisa yana mahitaji mengi na DP ameyasaidia sana ,amesema Askofu huyo .
“ Iwapo naibu wa rais atakuja katika kanisa langu nitafurahi sana kumpokea kwa moyo wote .kama kiongozi wa waumini wangu najua hatuna ala za muziki ,viti na tuna mahitaji mengi ambayo naibu wa rais anaweza kutusaidia’ amesema
Matamshi yake yalikaririwa pia na Askofu John Korir a mhubiri Joseph Too . Wamesema wale wanaomshtumu Ruto kwa ufisadi hawana uwezo wa kumtolea hukumu na badala yake wanafaa kujiunga naye kuifanya kazi ya Mungu .