Baada ya video yake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii akitimua mbio huku koti lake likipepea kutokana na kasi ya aliokuwa akikimbia, Seneta Irungu Kang’ata ameelezea sabu ya yeye kutimua mbio siku ya Jumapili katika mkutano wa Naibu Rais William Ruto.
Kwenye video iliyoenea siku ya Jumatatu, Kang'ata, ambaye alikuwa amevaa suti ya samawati na shati nadhifu alionekana akikimbilia kwenye ibada ambayo Ruto alikuwa akihudhuria katika kaunti ya Murang’a.
Kang’ata ambaye wiki chache zilizopita alitemwa kutoka wadhifa wa kiranja wa wengi katika Seneti alionekana akichana mbuga na kuacha mlinzi wake nyuma akijikokota kumfikia.