In Summary
  • Aliyekuwa mbunge wa Kibwezi Kalembe Ndile kuzikwa Juni 11
  • Ndile alifariki Jumapili asubuhi katika Hospitali ya Nairobi baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa ini
kalembe.ndile.

Mbunge wa zamani wa Kibwezi Kalembe Ndile atazikwa Juni 11 nyumbani kwake Mbui Nzau katika Kaunti ya Makueni.

Ndile alifariki Jumapili asubuhi katika Hospitali ya Nairobi baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa ini.

Mbunge wa Mavoko Patrick Makau alitangaza tarehe ya mazishi Jumatano baada ya kuhudhuria mkutano wa maandalizi ya mazishi katika nyumba nyingine ya Ndile huko Greepark Estate huko Machakos.

Makau aliwahimiza wanasiasa kuchangia kwa uzuri kumpa mwenzao heshima ya mwisho.

Ndile ametsifiwa kama mwanaharakati wa haki asiyeogopa na viongozi kadhaa wa Makueni.

Walimtaja mbunge huyo wa zamani kama mtu mkarimu na mwanaharakati hodari wa haki za binadamu.

Ndile alizaliwa Magharibi mwa Uganda mnamo 1964 kutoka ambapo alipata jina la utani la Kalembe.

Alisema jina lake maarufu Kalembe lilikuwa jina la utani lililochukuliwa kutoka kwenye migodi ya Kalembe.

View Comments