Kundi la mwisho la sindano maalum kutumiwa kwa chanjo za Pfizer liliwasili nchini siku ya JUmapili asubuhi.
Hii sasa inakamilisha kundi la sindano maalum milioni 2.2 kutoka kwa serikali ya Marekani ambayo itatumika katika kusimamia chanjo.
Wizara ya Afya inasema sasa itaanza kupeana chanjo ya Pfizer kuanzia Jumatatu.
Hii inatarajiwa kuongeza mpango wa chanjo ambayo inalenga kuwa Wakenya milioni 10 ifikiapo mwezi wa Desemba mwaka huu.
Kenya ilipata kundi la kwanza la sindano maalum siku ya Jumamosi.