26 April 2022 1 Min Read
Matiang'i atangaza Jumanne sikukuu ya umma kusherehekea Idd
In Summary
- Matiang'i atangaza Jumanne sikukuu ya umma kusherehekea Idd
Waziri wa Mambo ya Ndani Fred Matiangi ametangaza Jumanne kuwa sikukuu ya kusherehekea Idd-ul-Fitr.
Katika notisi ya gazeti la serikali mnamo Jumanne, Matiang'i alitangaza Mei 3 kuwa sikukuu ya umma kwa kutekeleza mamlaka yaliyotolewa na kifungu cha 2 (1) cha Sheria ya Likizo ya Umma.
Sikukuu ya Idd-ul-Fitr, Sikukuu ya Kufungua Mfungo, ni sikukuu muhimu ya kidini inayoadhimishwa na Waislamu ulimwenguni kote ambayo inaadhimisha mwisho wa Ramadhani, mwezi mtukufu wa Kiislamu wa mfungo.
Waislamu husherehekea Idd-ul-Fitr kwa sala zinazoitwa "Salat Al Eid" kwa Kiarabu.