Rais Trump arejea katika kampeini baada ya 'kupona' corona
Bila Maski! Trump arejelea kampeini Florida baada ya kuondoka Hospitalini
Analenga kushinda kura za Florida ili kutetea kiti chake
- Daktari wa Trump amesema hawezi kuambukizwa watu covid 19
- Rais Huyo amekataa kufanya mdahalo kupitia njia ya mtandao na mpinzani wake Biden
Rais wa Marekani amerejea tena katika kampeini chini ya wiki mbili tangu alipopatikana na virusi vya corona .
Maelfu walikuwanyika katika mkutano wake huko Sanford ,Florida ambako Trump alifanya mkutano mmoja kati ya msururu wa mikutano mine ya kampoeini anapolenga kukitetea kiti chake katika uchaguzi wa tarehe 3 Novemba
Siku ya jumatatu mpinzani wa Trump Joe Biden alikuwa katika jimbo la Ohio mbalo linatajwa kuwa muhimu kwa yeyote anayelenga kukishinda kiti hicho .
Kura ya maoni inaonyesha kwamba Biden ameunda pengo la alama kumi na Bwana Trump .
Baadhi ya majimbo ni muhimu sana kwani ndio yenye usahuwisho kuhusu kura za wajumbe 270 ambazo mtu anahitaji ili kukinyakuwa kiti cha urais .
Trump alipatikana na virusi vya corona siku 11 zilizopita na kulazwa hospitalini siku moja baadaye . Siku ya jumapili daktari wake alisema Trumo amepona virusi hivyo na hayupo katika hatari ya kuwaambukiza watu wengine .
Kundi lake la kampeini limeamua kuingia Florida kwa kishindo kwa sababu akizpoteza kura za eneo hilo huenda akapata ugumu wa kurejea White House .