In Summary

 

  •  Wivu wa kupundukia katika mapenzi ni hatari 
  •  Kuna mipaka ambayo hufai kuvuka katika uhusiano 
  •  Mtu asiyekuamini hafa kuwa nawe katika uhusiano 
  •  wivu wa mapenzi unafaa kuwa unaoeweka wala sio wa kutisha 

 

 

Wakati unapokutana na mtu anayekuvutia ambaye unatamani kuwa naye katika mahusiano , matumaini huwa kwamba ni mtu wa kuelewa na ambaye ataheshimu mipaka na  ‘uhuru’ wako hata ndani ya mahusiano yenu .

 Lakini hebu jiweke katika taswira hii ambapo mpenzi wako hakuruhusu hata kwenda dukani pekee yako ,hakuruhusu kuzungumza na mwanamke yeyote na hata akiwa ni mwanamke jamaa yake basi mpenzi wako ananuna .

 Ndio masaibu ya Elvis   ambaye uhusiano wake na  Anita  umekuwa jela kwani hana  uhuru wake  na hata amani  hana katika uhusiano wao . Wakati Anita anaposafiri kwenda  kwao , sarakasi huzidi na kuwa maradufu kwa sababu wakati wote anapiga simu akimuuliza  Elvis kwamba afanya nini na yuko wapi na yuko na nani . Elvis anasema wakatia mwingine imekuwa vigumu kuendelea na shughuli zake za kikazi kwa sababu ya kuvurugwa fikra kila wakati na mpenzi wake . Cha kushangaza ni kwamba anaporejea ,Anita hushtukiza tu  na kuingia chumbani  masaa ya kutisha kama siku moja alivyorejea nyumbani mwendo wa saa kumi alfajiri . Lengo lilikuwa kumpata Elvis akiwa na mwanamke mwingine chumbani .

 

 Licha ya kuwa hakupata jambo lolote la kuzua shauku ,alifanya ukaguzi nyumba nzima hadi mvunguni mwa kitanda kabla ya kutulia .  Elvis amesema  jaribio lake la kumpa hakikisho Anita kwamba hana uhusiano mwingine wala  nia ya kujihusiaha na mpenzi wa pembeni ,Anita  hajatulia na wivu wake wa kimapenzi hata umevurugisha mahusiano yao na rafiki zao .

 Elvis anapopokea simu hata ya mamake au mtu yeyote wa kike ,ni sharti aweke kwenye spika ili Anita ajue anazungumza na nani na asipofanya hivyo basi hawatazungumziana kwa wiki kadhaa 

 Anasema jaribio lake la kumtaka Anita apate usaidizi wa mshauri ili uhusiano wao uwe wa kawaida limegonga mwamba kwani pendekezop  hilo kila mara linafuatwa na kununa na  maandamano pamoja na mgomo baridi wa kimya chumbani huku wakikosa kuzungumziana .

 Kama kuna  wakati Elvis alitaka kusalimu amri kuhusu uhusiano wake na Anita bsi ni siku ambayo Anita alichukua simu yake ya mkononi na kumpigia bosi wake kazini na kumtaka akome kuzungumza na Elvis kwa sababu alikuwa ameona jumbe kati yao kuhusu masuala ya kikazi lakini hilo halikutosha kumfanya ajue kwamba hamna cha ziada kati yao ila kazi .

 Elvis anasema hawezi kukumbuka ni mara ngapi Anita amefungisha virago  kwenda kwao na wiki oja hata haishi  kabla hajarejea na hata kuapa kwamba hatorudia sarakasi zake lakini hilo huwa tu ahadi kwani hajabadilika  hata kidogo .

 Je  ,ni kiwango kipi cha wivu wa kimapenzi ambacho mtu anaweza kustahmili?

 

View Comments