30 July 2021 1 Min Read
Mke wa naibu gavana apatikana amefariki ndani ya nyumba
Masud ambaye ni mzaliwa wa nchi ya Tanzania amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya moyo kwa muda.
In Summary
•Mkewe Saisi, Ashura Masud Saisi alipatikana akiwa ameaga ndani ya nyumba na mmoja wa watoto wake.
Naibu gavana wa kaunti ya Vihiga Patrick Saisi alipoteza mkewe Alhamisi alasiri.
Mkewe Saisi, Ashura Masud Saisi alipatikana akiwa ameaga ndani ya nyumba na mtoto wake mmoja.
Masud ambaye ni mzaliwa wa nchi ya Tanzania amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya moyo kwa muda.
Msaidizi wa naibu gavana huyo alithibitisha taarifa hizo kwa simu.