In Summary
  • Mnamo Septemba, kiongozi huyo wa Wiper alipuuzilia mbali madai kwamba aliwasiliana na Rais
  • Kalonzo alisema uvumi huo kwenye mitandao ya kijamii ni ubunifu wa watu wenye nia mbaya
  • Alisema atakutana na Ruto hadharani kwa wakati ufaao, lakini baada ya kushauriana na uongozi wa Wiper na Azimio
Image: EZEKIEL AMING'A

Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka alihudhuria sherehe za Mashujaa Day katika bustani ya Uhuru Gardens.

Huenda alikuwa kiongozi pekee wa Muungano wa Azimio la Umoja One aliyehudhuria sherehe za 59 za Mashujaa Day.

Kalonzo aliketi kwenye jukwaa la watu mashuhuri na hata alilakiwa na Rais William Ruto alipofika.

Mnamo Septemba, kiongozi huyo wa Wiper alipuuzilia mbali madai kwamba aliwasiliana na Rais.

Kalonzo alisema uvumi huo kwenye mitandao ya kijamii ni ubunifu wa watu wenye nia mbaya.

Alisema atakutana na Ruto hadharani kwa wakati ufaao, lakini baada ya kushauriana na uongozi wa Wiper na Azimio.

Wiki iliyopita, Kalonzo alimsihi Rais afikirie upya msimamo wake kuhusu kuondoa marufuku ya vyakula vya GMO nchini.

Kuwepo kwake kulikuja kwa mshangao, kutokana na msimamo wake wa awali kwamba Azimio hatajihusisha na serikali kwa njia nyingine yoyote isipokuwa kuidhibiti.

Aidha iliibua uvumi iwapo kinara wa chama cha muungano huo Raila Odinga, ambaye yuko nje ya nchi kwa safari ya siku 10 , alifahamu kuwa alikuwa akihudhuria hafla hiyo.

 

 

 

View Comments