logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Safaricom sasa imesema bonga points sasa zitakatwa kulipa okoa jahazi

Safaricom sasa watakata bonga points ili kulipa okoa jahazi.

image
na

Makala08 March 2023 - 05:44

Muhtasari


Bonga points huzawadiwa mteja alama 1 kila anapotumia shilingi kumi ya muda wa hewa na wateja wanweza kuipata muda wa hewa shilingi 3 kwa alama 10,muda wa hewa wa shilingi 8 kwa alama 25 au kununua data ya mtandao kutumia alama hizo.

Afisa mkuu mtendaji wa Safaricom Peter Ndegwa akizindua programu ya M-Pesa mnamo Juni 23, 2021.

Watumizi wa Safaricom wanaochelewa kulipa deni la okoa jahazi sasa watalipa deni lao kiotomatiko iwapo watakuwa na bonga points.Hatua hii imechukuliwa na Safaricom ili kuhakikisha matumizi ya mabilioni ya bonga points na kuishusha thamani yake.

Hatua hiyo pia itatahakikisha kuwa wale wanaopitiza masiku za kulipa deni lao la okoa jahazi wamelipa kutolewa kwa bonga points ili kilipa deni.

Mwishoni mwa mwaka uliopita,Safaricom ilitangaza kuwa watu waliokuwa na bonga points watakatiziwa bonga points mwanzoni mwa mwaka wasipotumia na kwamba huduma hii itakuwa na muda wa kuisha kinyume na hapo awali ambapo bonga points haikuwa na muda wa kuisha.

Tangazo hilo lilizua hisia tofauti huku wateja wa Safaricom wakipinga na kulalamikia Safaricom kwa kuweka muda wa kuisha kwa bonga points hatua iliyoifanya Safaricom kufutilia mbali tangazo hilo.

Bonga points huzawadiwa mteja alama 1 kila anapotumia shilingi kumi ya muda wa hewa na wateja wanweza kuipata muda wa hewa shilingi 3 kwa alama 10,muda wa hewa wa shilingi 8 kwa alama 25 au kununua data ya mtandao kutumia alama hizo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved