In Summary

 

  •    Kaunti za  Makueni na Kakamega zafurahia sana ugatuzi 
  • Tana River na Taita Taveta zasema hazijafurahia ugatuzi

 

Ripoti: Utafiti wa maoni kuhusu waknya kuridhishwa na ugatuzi
Image: Infotrak

 

Asilimia 73 ya wakenya wanahisi kwamba ugatuzi umeleta mabadiliko katika maeneo ya  mashinani ikilinganishwa na kabla ya kuanza kwa mfumo huo wa utawala . Kwa mujibu wa utafiti wa kura ya maoni uliofanywa na kampuni ya Infotrak  asilimia 15 ya waknya hata hivyo wanasema hali imekuwa mbaya Zaidi kuliko hapo awali ilhali asilimia 12 wanasema hapajakuwa na mabadiliko yoyote .

Wakaazi wengi wa kaunti za Makueni na Kakamega kwa asilimia 90 ndio wanaosema kwamba kumekuwa na mabadiliko makubwa sana yaliyosababishwa na ugatuzi .

 
 

 Kaunti nyingine zinazofurahia ugatuzi ni  Turkana  na West Pokot kwa kwa asilimia 87, Machakos kwa asilimia 86 , Kericho kwa  asilimia 82 ,Mandera  Bomet ,kisumu na Uasin Gishu  kwa asilimia 81  na Elgeyo Marakwet  na Kisii kwa asilimia 80 .

 Kaunti ambazo wakaazi hajawaona tofauti ni Taita Taveta kwa asilimia 48, Tana River kwa asilimia 56 ,Kiambu kwa asilimia 56 ,Homabay kwa asilimia 57  na Trans Nzoia kwa asilimia 58 .

Jumla ya watu 37,600 kote nchini walihojiwa katika utafiti huo wenye  uhakika wa asilimia 95

 

View Comments