In Summary

 

  •  Sumbi alihamishwa hadi Bungoma ili baada ya hali yake kudhoofika 
  • Oparanya amemtaja kama mchapa kazi na rafiki yake  wa karibu 

 

 

Marehemu Robert Sumbi

 

Gavana wa kakamega Wycliffe Oparanya  ameomboleza kifo cha afisa mkuu wa wafanyikazi katika kaunti hiyo aliyekuwa akiugua virusi vya corona .

Robert Sumbi  aliaga dunia siku ya alhamisi katika  hospitali ya  Life Care mjini Bungoma  ambako alikuwa amehamishwa kutoka hospitali ya kaunti ya kakamega  baada ya hali yake kuzoto siku ya jumatano .

 Ni miongoni mwa maafisa wakuu wa kaunti waliopata ugonjwa huo katika siku za hivi karibuni

"Sumbi  alikuwa mtu aliyejitolea ,mchapa kazi ,mtu mkweli na aliyekuwa  mchango mkubwa sana ‘amesema Oparanya

 Kupitia taarifa ,oparanya amesema kifo cha Sumbi ni pigo kubwa kwa serikali ya kaunti ya kakamega

" Tumempoteza mtu aliyekuwa na maono na ambaye mchango wake utakosekana sana .  nimempoteza rafiki na mshirika wa karibu  ambaye ushauri  na msaada wake ulinisaidia katika kufanya maamuzi muhimu’amesema Oparanya .

Sumbi  alifaa kufanyiwa dialysis  kwa ajili alikuwa na maradhi ya figo  na hangeweza kuhudumiwa katika  hospitali kuu kwa sababu ya kuwa na virusi vya corona .

" Tulilazimika kumhamisha hadi Bungoma  kwani wangeweza kumfantyia dialysis na kumweka katika kitengo cha ICU  kwa sababu vitanda vyetu vya ICU hapa vina  wagonjwa wengine wa corona’amesema daktari mmoja

Sumbi alihudumu kama waziri wa kaunti wa mazingira na maji kati ya mwaka wa 2013 na 2017 .Alitajwa kuwa mkuu wa utumishi wa wafanyikazi  baada ya Oparanya kuchaguliwa tena mwaka wa 2017

 

 

View Comments