Last Updated On 19 November 2020 1 Min Read
Korti yaagiza kufunguliwa kwa shule
Mahakama yapiga marufuku masomo ya kijamii na kuagiza shule kufunguliwa katika siku 60
Jaji asema Magoha hana mamlaka ya kuagiza kufungwa kwa shule
Jaji mmoja ameagiza kufunguliwa kwa shule zote katika 80 zijazo na kupiga marufuku masomo yanayotolewa kijamii yalioanzishwa na serikali .
Jaji James Makau pia amesema waziri wa elimu George Magoha hana mamlaka ya kuagiza kufunguliwa kwa shule chini ya sheria ya elimu ya msingi .
Jaji amesema waziri Magoha anafaa kuhakikisha kwamba shule zinafunguliwa na kuweka mikakati ya kuhakikisha kwamba kanuni za wizara ya afya kuhusu kuzuia maambukizi ya corona zinatekelezwa .
Katika uamuzi wake jaji amesema serikali ilikiuka haki za wanafunzi na kukosa kuonyesha jinsi masomo ya kijamii yalivyo halali kwa mujibu wa sheria . Uamuzi huo umetokana na kesi iliyowasilishwa na Joseph Enock Aura .