Korti yaagiza kufunguliwa kwa shule

Mahakama yapiga marufuku masomo ya kijamii na kuagiza shule kufunguliwa katika siku 60

Jaji asema Magoha hana mamlaka ya kuagiza kufungwa kwa shule

Waziri wa Elimu George Magoha

Jaji mmoja ameagiza kufunguliwa kwa shule zote katika 80 zijazo na kupiga marufuku masomo yanayotolewa kijamii yalioanzishwa na serikali .

 Jaji James  Makau  pia amesema waziri wa elimu  George Magoha  hana mamlaka ya  kuagiza kufunguliwa kwa shule chini ya sheria ya elimu ya msingi .

 Jaji amesema waziri  Magoha  anafaa kuhakikisha kwamba shule zinafunguliwa  na kuweka mikakati ya kuhakikisha kwamba kanuni za wizara ya afya kuhusu kuzuia maambukizi ya corona zinatekelezwa .

  Katika uamuzi wake jaji amesema serikali  ilikiuka haki za wanafunzi  na kukosa kuonyesha jinsi masomo ya kijamii yalivyo halali kwa mujibu wa sheria . Uamuzi huo umetokana na kesi iliyowasilishwa na Joseph Enock Aura .