Watu 1,048 wamepatikana na virusi vya corona baada ya sampuli 8,660 kupimwa katika saa 24 zilizopita na kufikisha 75,193 jumla ya visa hivyo nchini huku sampuli zilizopimwa zikiwa 823,700 . Kutoka visa hivyo 1,018 ni wakenya ilhali 30 ni raia wa kigeni .watu 594 ni wanaume ilhali 454 ni wanawake .Mgonjwa wa umri wa chini ni mtoto wa mwaka mmoja ilhali wa umri wa juu ana miaka 90
Leo watu 326 wamepona na kufikisha 50,984 idadi ya watu waliopona ugonjwa huo hadi kufikia sasa .