In Summary

 

  •  Amekuwa ICU kwa siku 10 tangu kuambukizwa ugonjwa huo 
  •  Alikuwa mkuu wa kitengo cha maradhi ya figo KNH 

 

Dr.Anthony Were

 

Mkuu wa kitengo cha kutibu maradhi ya figo katika hospitali ya Kenyatta Dr Anthony Were Omolo  amefariki kutokana na  virusi  vya corona

Dr Were  aliaga dunia siku ya ijumaa usiku baada ya kuwa katika kitengo cha ICU kwa siku 10  ambapo amekuwa akipokea matibabu  baada ya kuambukizwa ugonjwa huo .

 

 Muungano wa madaktari umemtaja Were kama mwalimu na mtu aliyekuwa kielelezo kwa madaktari wengi . KMPDU imetuma risala  za rambi rambi kwa familia yake .

 

View Comments