Jaji Mkuu mpya
Idara ya mahakama yaanza kumsaka Jaji mkuu mpya
Mtu atakayefaulu kupewa kazi hiyo atakuwa na mshahara wa kati ya shilingi 990,000 na 1,327,888 bila kujumuisha marupurupu .
- Mshikilizi wa nafasi hiyo ana jukumu la kuongoza iadara ya mahakama ambayo ni kitengo cha tatu cha serikali na atahudumu pia kama mwenyekiti wa JSC na rais wa mahahakama ya juu zaidi
- Mwaka wa 2016 Maraga aliwapiku watu wengine 13 kumrithi Willy Mutunga ambaye alistaafy mwaka mmoja mapema .
Idara ya mahakama imeanza kumtafuta jaji mkuu mpya ili kuiziba nafasi iliyoachwa wazi na David Maraga . kupitia arifa ya gazeti asmi la serikali iliyotiwa saini na kaimu jaji MKUU Philomena Mwilu ,hatua hiyo inajiri wiki mja baada ya Maraga kustaafu .
Notisi hiyo inawaalika wanaotaka kuhudumu katika nafasi hiyo kutuma maombi ili kuzingatiwa na tume ya huduma kwa idara ya mahakama .
Wanaotuma maombi wanafaa kuwa mawakili wa mahakama kuu na uzoefu wa miaka 15 au kuwa jaji wa mahakama kuu au ya rufaa au afisa wa idara ya mahakama na uzoefu na elimu inayotesheleza matakwa ya mshikilizi w anafasi hiyo .
Miongoni mwa watu walioonyesha nia ya kutaka nafasi hiyo ni mkurugezi wa zamani wa mashtaka ya umma Philip Murgor . wengine ni naibu jaji mkuu Philomena Mwilu ,rais wa mahakama ya rufaa William Ouko ,mwanasheria mkuu Kihara Kariuki na mtangulizi wake Githu Muigai .
Mtu atakayefaulu kupewa kazi hiyo atakuwa na mshahara wa kati ya shilingi 990,000 na 1,327,888 bila kujumuisha marupurupu .
Mshikilizi wa nafasi hiyo ana jukumu la kuongoza iadara ya mahakama ambayo ni kitengo cha tatu cha serikali na atahudumu pia kama mwenyekiti wa JSC na rais wa mahahakama ya juu zaidi
Mwaka wa 2016 Maraga aliwapiku watu wengine 13 kumrithi Willy Mutunga ambaye alistaafy mwaka mmoja mapema .