In Summary

•Kufikia vurugu hiyo, George Koimburi alikuwa anaongoza kwa asilimia sabini na saba.
•Mbunge wa Gatundu Kusini, Moses Kuria adai kunusurika kifo kwa upeo.

Kituo cha kupigia kura Juja
Image: Hisani: The Star

Shughuli ya kuhesabu kura katika eneo bunge la Juja imesitishwa kwa muda.

Hii ni baada cha kikundi kinachodaiwa kuongozwa na gavana wa Kiambu James Nyoro kuvamia kituo cha kuhesabu kura cha mang'u na kusababisha vurugu.

Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, IEBC ilikashifu sana tendo hilo la uhuni ambalo lilifanya shughuli hiyo kuwa ngumu kuendelea."Ili kulinda maafisa wetu, vifaa vinavyotumika kwenye uchaguzi na uadilifu wa shughuli ya uchaguzi, tume hili linasitisha shughuli ya uhesabu kura na matokeo yatatangazwa hali ya kawaida ikirejea" IEBC ilitangaza.
ujumbe wa iebc
Image: HISANI

Hata hivyo, tume hilo lilitangaza kuwa vifaa vyote na matokeo yaliyokuwa yamefika yako salama. IEBC iliwasihi wagombea kiti wote kuwa wenye utulivu hadi matokeo yatakapotangazwa.

Kufikia kutokea kwa vurugu hiyo, mgombea kiti kwa tikiti ya PEP, George Koimburi alikuwa anaongoza kwa asilimia sabini na saba huku akifuatwa nyuma kwa umbali na Susan Njeri wa Jubilee.

Kupitia ujumbe wa Facebook, mbunge wa Gatundu ya Kusini alieleza masaibu yaliyowakumba wakiwa na Koimburi wakati wa vurugu hiyo."Sasa ni 3.42AM na bado tumekwama katika kituo cha Mang'u. Hatuna uhakika wakati tutakapotoka kwenye kituo hiki. Tunawaomba Wakenya mutuombee. Jana usiku tulinusurika kifo na hiyo ni ishara kuwa Mungu yu nasi" Kuria aliandika.

View Comments