Watu 258 wamepatikana na maambukizi ya Covid-19 kutoka kwa sampuni 3,137 chini ya saa 24 zilizopita.
Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 241 ni wakenya ilhali 17 ni raia wa kigeni,142 ni wanaume huku 116 wakiwa wanawake.
Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 240,430 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 8.2%.
Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,414,857.
Mgonjwa wa umri wa chini ana miezi 3, huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 102.
Kwa habari za kuhuzunisha watu 9 wameaga dunia kutokana na virusi vya corona, na kufikisha idadi jumla ya 4,795 ya walioaga dunia.