Wakati wa patashika hiyo, Kamotho alijeruhiwa mkono wake wa kushoto na tumbo na akukimbizwa hospitali ya Nile kupata matibabu.
Katika harakati za kutoroka, afisa mmoja - Inspekta Soita alipoteza simu yake ya mawasiliano ya polisi, ambayo ilipatikana na polisi waliokuwa katika doria ambao walikuwa wamewasili kudhibiti hali.
"Maafisa wa polisi waliokuwa doria huko Kikuyu, walikimbilia eneo la tukio na kufanikiwa kutuliza hali na kuchukuwa kifaa muhimu cha mawasiliano cha polisi."
Uchunguzi wa awali ulifichua kwamba kifaa hicho cha mawasiliano kilikuwa kimepewa Soita, ambaye ndiye msimamizi wa kituo cha Doria cha Lower Kabete.
Maafisa hao wawili walikamatwa, wakapokonywa silaha na kuwekwa chini ya ulinzi katika kituo cha polisi cha Gigiri.
Watafikishwa mahakamani.