logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi 2 wakamatwa kwa jaribio la wizi wa mabavu

Uchunguzi wa awali ulifichua kwamba kifaa hicho cha mawasiliano kilikuwa kimepewa Soita, ambaye ndiye msimamizi wa kituo cha Doria cha Lower Kabete.

image
na Radio Jambo

Habari09 September 2021 - 14:01

Muhtasari


Katika harakati za kutoroka, afisa mmoja aliangusha simu yake ya mawasiliano ya polisi, ambayo ilipatikana na polisi waliokuwa katika doria.

Uchunguzi wa awali ulifichua kwamba kifaa hicho cha mawasiliano kilikuwa kimepewa Soita, ambaye ndiye msimamizi wa kituo cha Doria cha Lower Kabete.

Maafisa wawili wa polisi wamekamatwa kwa tuhuma za jaribio la wizi wa mabavu katika eneo la Kioko, Dagoretti.

Kulingana na Kurugenzi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai, maafisa hao waliotambuliwa kama Inspekta Evans Soita na Konstebo John Kemboi waliingia kwenye duka la Stephen Kamotho huko Dagoretti saa tano asubuhi siku ya Jumatano na makabiliano yakaanza.

Maafisa hao wanaohudumu katika kituo cha Polisi cha Spring Valley kisha walimtishia mwenye duka kwa bunduki na kujaribu kumuweka pingu.

 Kamotho kisha alipiga kamza na wananchi wakaja kumwokoa kutoka kwa maafisa hao.

"Walipoona wamezingirwa na wananchi, maafisa hao waliamua kutoroka kwa kupiga risasi moja angani ili kuogofya umati huo uliokuwa na hamaki," DCI alisema.

Wakati wa patashika hiyo, Kamotho alijeruhiwa mkono wake wa kushoto na tumbo na akukimbizwa hospitali ya Nile kupata matibabu.

Katika harakati za kutoroka, afisa mmoja - Inspekta Soita alipoteza simu yake ya mawasiliano ya polisi, ambayo ilipatikana na polisi waliokuwa katika doria ambao walikuwa wamewasili kudhibiti hali.

"Maafisa wa polisi waliokuwa doria huko Kikuyu, walikimbilia eneo la tukio na kufanikiwa kutuliza hali na kuchukuwa kifaa muhimu cha mawasiliano cha polisi."

Uchunguzi wa awali ulifichua kwamba kifaa hicho cha mawasiliano kilikuwa kimepewa Soita, ambaye ndiye msimamizi wa kituo cha Doria cha Lower Kabete.

Maafisa hao wawili walikamatwa, wakapokonywa silaha na kuwekwa chini ya ulinzi katika kituo cha polisi cha Gigiri.

Watafikishwa mahakamani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved