Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma imekanusha madai kwamba inarudisha nyuma uchunguzi wa kesi za ufisadi katika shirika la Kemsa.
Katika taarifa siku ya Alhamisi, Naibu DPP Emily Kamau alisema ofisi ya DPP inashirikiana na Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa kumaliza kukamilisha kesi hiyo.
Kamau alikuwa akijibu madai katika taarifa ya Citizen TV ambayo ilidai kuwa DPP bado hajarudisha faili ya kesi hiyo kwa EACC mwaka mmoja baada ya kutoa ahadi ya kufanya hivyo.
EACC ilipeleka faili hiyo kwa DPP ikipendekeza mashtaka dhidi ya maafisa sita wa Kemsa.
Akijibu madai hayo, Kamau alisema ofisi ya mkurugenzi wa mshtaka ilirudisha faili hiyo kwa EACC baada ya kubaini eneo la uchunguzi zaidi.
"Ripoti ya Citizen TV haikuwa sahihi, mbaya na ya kupotosha, kwani ni dhahiri kazi nyingi zimekuwa zikiendelea katika uchunguzi wa Kemsa," Kamau alisema.