Ushauri umetolewa kufanyika kwa mashauriano ya kina kati ya Bodi simamizi za Shule (BOM), wazazi na Wizara ya Elimu kushughulikia suala ya machafuko shuleni.
Mwakilishi wa Wanawake wa Migori Pamela Odhiambo ametaka mazungumzo hayo kufanyika haraka iwezekanavyo. Akizungumza mwishoni mwa wiki Odhiambo alibainisha kuwa ni jambo la kuhuzunisha kuona wanafunzi wakichoma shule, taasisi ambazo zinazopaswa kuwafinyanga kuwa viongozi wanaowajibika siku zijazo.
Mwakilishi huyo wa wanawake alisema wasimamizi wa shule wanapaswa kujitahidi kila wakati kujua kile ambacho wanafunzi walitaka badala ya kile wanachohitaji.
“Wakati mwingine si vibaya kuwasikiliza wanafunzi kuhusu masuala mbalimbali ambayo yanaweza kuwaathiri. Ni bora kujadiliana na wanafunzi hawa na kuwa na kuweka mikakati ya kuzuia badala ya kuwapuuza na kujuta baadaye, "alisema.