In Summary

•Katibu wa One Kenya  amesema kikao hicho na wanabahabari ambacho kimetabiriwa kufanyika mwendo wa saa 10 asubuhui kitahudhuriwa na vinara  wote wa OKA

•Vinara hao ni ikiwemo na Musalia Mudavadi wa ANC, Moses Wetang'ula wa Ford Kenya, Kalonzo Musyoka wa Wiper, Gideon Moi wa KANU

Viongozi wa OKA Moses Wetang'ula, Kalonzo Musyoka na Gideon Moi wakati wa ibada ya kumuaga Mama Rosebella Jerono Mudavadi katika Kanisa la Friends Church-Quakers mnamo Desemba 16.
Image: MERCY MUMO

Vinara wa Muungano wa One Kenya  wanatarajiwa kuhutubia wanahabari Jumatano asubuhi kufuatia habari za  kuongezeka kwa mpasuko wa  muungano huo 

Katibu wa One Kenya  amesema kikao hicho na wanabahabari ambacho kimetabiriwa kufanyika mwendo wa saa 10 asubuhui kitahudhuriwa na vinara  wote wa OKA

Vinara hao ni ikiwemo na Musalia Mudavadi wa ANC, Moses Wetang'ula wa Ford Kenya, Kalonzo Musyoka wa Wiper, Gideon Moi wa KANU.Cyrus Njirongo anatarajiwa kuhutubia umma pia 

Mkutano huo wa dharura umeandaliwa baada ya Naibu Rais, William Ruto kuonekana akiwa na mpango wa kufanya kazi pamoja na baadhi ya vinara wa muungano wa OKA.

Isitoshe pia, kinara wa ODM, Bw Raila Odinga ameokana  kwa ukaribu sana na seneta wa Baringo, Gideon Moi, ambaye siku ya mkutano wa Azimio la Umoja alihudhuria  mkutano ulioandaliwa Kasarani wa Azimio  la umoja 

Baadhi ya vinara Ruto analenga kuwavuta kurtoka mrengo huo,  ni ikiwemo na Musalia mudavadi na seneta Moses Masika Wetang'ula

 

View Comments