Mchanganuzi wa masuala ya kisiasa, Herman Manyora amewaomba rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto kukoma kutupiana maneno makali wanapokuwa katika majukwaa ya kampeni.
Akizungumza kupitia video aliyopakia katika akaunti yake ya YouTube, Manyora amesema kwamba wawili hao wanapaswa kuwaheshimu wananchi wanaowaongoza na kukoma kuonyesha chuki zao waziwazi kwa umma na badala yake kuangazia maendeleo kwa wananchi.
Manyora amemsihi naibu rais William Ruto kumheshimu rais Kenyatta pamoja na ofisi yake na kusubiri wakati wake ambapo atafanikiwa kuchaguliwa kuwa kiongozi wa taifa.
Kulingana na mchanganuzi huyo, uhusiano wa rais na naibu wake ulisambaratika katika awamu yao ya kwanza walipoingia serikalini kupitia chama cha Jubilee.