30 April 2022 1 Min Read
Hatimaye Hayati Mwai Kibaki azikwa nyumbani kwake Othaya
In Summary
- Tukio la maziko lilikuwa la faragha; iliyohudhuriwa na familia na wageni wachache
Aliyekuwa Rais wa Kenya marehemu Mwai Kibaki amezikwa nyumbani kwake katika Eneo Bunge la Othaya, Kaunti ya Nyeri.
Tukio la maziko lilikuwa la faragha; iliyohudhuriwa na familia na wageni wachache.
Mwili wa Kibaki ulizikwa karibu na kaburi la mkewe Mama Lucy Kibaki.
Misa ya Mazishi ya Rais Mstaafu wa Kenya Mwai Kibaki ilihudhiriwa na wakenya wa tabaka mbali mbali
Ibada hiyo iliongozwa na Kanisa Katoliki ambalo marehemu alikuwa mshirika.
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya walihudhuria ibada hiyo