hACKED

Kenya imemwulikwa sana kutokana na kuripoti  visa vingi vya udukuzi wa mitambo ya tarakilishi pamoja na wizi wa pesa kwenye mashine za ATM mwaka huu, idadi ya visa hivyo ikiwa takribani vitano jambo linalosemekana kuendelezwa na  wahalifu wa mitandao.

Wezi stadi wamefanikiwa kutoroka na mamilioni ya fedha kwa kudukua mashine za ATM. Udukuzi huu unajumuisha kueneza programu kwenye mitambo ya pesa na kusababisha kutoa kiasi kikubwa cha hela kwa mkupuo moja.

Akizungumza katika kongamano la uslama wa kimitandao na matumizi ya intaneti, Waziri wa usalama wa ndani Fred Matiang'i alisema kwamba kumekuwa na ongezeko la visa vya uhalifu mitandaoni, visa vya ulaghai kutoka watu bandia mtandaoni, usambasaji wa programu hasidi kwenye intaneti, udukuzi, na wizi wa kimitandaoni.

Visa hivi vimeweka Kenya katika ngazi ya juu kutokana na utovu wa usalama wa mitandaoni.

Kampuni  inayotoa huduma za kudhibiti programu hasidi Kaspersky Security Network (IT Threat Evolution Quarter Two 2019) imeorodhesha taifa la Kenya kuwa miongoni mwa mataifa 10 yanayokabiliwa na athari hiyo.

Iran inaongoza kwa asilimia 28.31, ikifuatwa na Bangladesh kwa silimia 28.1 huku Kenya ikiwa nambari 10 kwa asilimia 15.38.

Hii hapa ni orodha ya nchi zilizoripotiwa kuwa na utovu wa usalama kwenye mitandao.

Asilimia

Nchi  %
1 Iran 28.31
2 Bangladesh 28.10
3 Algeria 24.77
4 Pakistan 24.00
5 Tanzania 23.07
6 Nigeria 22.69
7 India 21.65
8 Indonesia 18.13
9 Sri Lanka 15.96
10 Kenya 15.38

Zaidi ya visa milioni 26.6 viliripotiwa kati ya Aprili na Juni mwaka huu kulingana na  Kituo cha Kitaifa cha kudhibiti visa vya mitandaoni.

View Comments