Mchuano kati ya mashetani wekundu na Leipzig ilisubiriwa sana na mashabiki wa kandanda huku Man United wakiibuka washinda kwa kuwachapa RB Leipzig tano kwa nunge.
Bao la Mason Greenwood, hat-trick ya Marcus Rashford na mkwaju wa penalti wa Anthony Martial uliwatosha Mashetani Wekundu kuendeleza kampeni yao ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu huu bila kichapo.
Ni mechi ambayo ilianza timu zote zikiwa na matumaini ya juu huku matumaini ya Leipzig yakitulizwa baada ya dakika 21 hii ni baada ya Paul Pogba kushirikiana na Greenwood ambaye alifunga bao la kwanza la mechi hiyo.