Beki matata Thiago Silva sasa atasalia katika klabu ya Chelsea hadi msimu ujao wa 2022/23.
Mbrazili huyo mwenye umri wa miaka 37 aliongeza mkataba wake na The Blues kwa mwaka mmoja mnamo Jumatatu, Januari 3, 2022.
Silva ambaye alijiunga na klabu hiyo mwaka wa 2020 ameendelea kushangaza wengi na fomu yake nzuri licha ya umri wake mkubwa.
Beki huyo ambaye amewakilisha The Blues katika mechi 56 kufikia sasa alisema anafurahia sana kuweza kuongeza mkataba wake pale.
"Kucheza hapa na Chelsea ni furaha ya kweli. Sikuwahi kufikiria ningecheza kwa miaka mitatu hapa katika klabu hii kubwa kwa hivyo nina furaha sana kubaki kwa msimu mwingine" Thiago alisema.