Kocha Aliou Cisse asifiwa kwa kuiongoza Senegal kutwaa taji la kwanza la Afcon
•Cisse amesifiwa kama kocha Mwafrika aliyeruka vikwazo vyote na kusaidia timu yake kunyakua mojawapo ya mataji makubwa zaidi duniani.
•Miongo miwili iliyopita, Cisse alikuwa nahodha wa kikosi cha Simba wa Teranga ambacho kilipoteza katika fainali ya Afcon dhidi ya Cameroon.
Kocha wa Senegal Aliou Cisse amepongezwa sana kufuatia ushindi wao wa taji la Afcon 2021 siku ya Jumapili.
Mchezaji huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 45 aliongoza taifa lake kunyakua taji la kwanza la Afcon kwa kuibwaga Misri katika fainali iliyochezwa ugani Yaoundé’s Olembe , Cameroon.
Miongo miwili iliyopita, Cisse alikuwa nahodha wa kikosi cha Simba wa Teranga ambacho kilipoteza katika fainali ya Afcon dhidi ya Cameroon.
Mchekeshaji mashuhuri Daniel Ndambuki almaarufu kama Churchill amemtambua Cisse kama gwiji kwa kusaidia taifa lake kunyakua taji la Afcon kama kocha baada ya kulikosa alipokuwa mchezaji.
"Gwiji huyu Aliou Cissé amenyanyua taji la Kombe la Afrika kama kocha baada ya kukosa kama mchezaji" Churchill alisema kupitia mtandao wa Twitter.