In Summary
  • Raila alionyesha imani kwamba wana ushahidi wa kutosha ambao unaona uamuzi wa Mahakama ya Juu kwa upande wao
Raila Odinga
Image: HISANI

Kiongozi wa Azimio Raila Odinga amezitaka nchi za kigeni kukoma kuingilia siasa za Kenya.

Kiongozi huyo wa Azimio alizitaka nchi za kigeni kusubiri hukumu ya Mahakama ya Juu ambayo imepangwa kusikiliza na kuamua kesi iliyowasilishwa mbele yake.

Raila alikuwa akihutubia taifa katika KICC Jumatatu baada ya kuwasilisha ombi la uchaguzi wa urais alipotoa matamshi hayo.

"Ata marafiki wetu kutoka ng'ambo ambao wako hapa, tungependa kuwasihi wawe na subira. Wasijiingize katika mambo ya siasa ya kindani ya Kenya. Waache Wakenya wasuluhishe mambo yako kama wakenya."

Raila alionyesha imani kwamba wana ushahidi wa kutosha ambao unaona uamuzi wa Mahakama ya Juu kwa upande wao.

"Tuna uhakika ya kwamba tuko na ushahidi wa kutosha kuonesha kuwa sisi ndio tulishinda uchaguzi wa 2022,"Alizungumza Raila.

Siku ya Jumatatu, Balozi wa Uingereza nchini Kenya Jane Marriott alikariri kwamba Uingereza na yeye mwenyewe hawakuwa na mgombea aliyependekezwa zaidi katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9, mwaka huu.

View Comments