15 August 2022 1 Min Read
(+Picha) Wakazi wa Kondele waanza sherehe kabla ya matokeo rasmi kutangazwa
"Tunataka kumwambia Chebukati kuwa tumekuwa na subira," alisema Omondi Okello,
In Summary
•Wenyeji walibainisha kuwa wamesubiri kwa muda mrefu na ni wakati ambao hatimaye matakwa yao yatatimizwa.
by FAITH MATETE Uchaguzi 2022
Wakaazi wa Kondele mjini Kisumu tayari wanasherehekea huku nchi ikisubiri mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati kutangaza matokeo ya urais.
Wenyeji waliozungumza na The Star walibainisha kuwa wamesubiri kwa muda mrefu na ni wakati ambao hatimaye matakwa yao yatatimizwa.
"Tunataka kumwambia Chebukati kuwa tumekuwa na subira," alisema Omondi Okello, mkazi.
Mkazi mwingine Mark Owino alisema, "Tunataka jambo hili lifikie mwisho ili tuweze kuendelea na biashara yetu."
- Wakazi wa Kondele waandamana hata kabla ya matangazo rasmi ya urais
- Wakazi wa Kondele waandamana hata kabla ya matangazo rasmi ya urais
- Wakazi wa Kondele waandamana hata kabla ya matangazo rasmi ya urais
- Wakazi wa Kondele waandamana hata kabla ya matangazo rasmi ya urais
Aliongeza kuwa pia wataendelea kuwa na amani bila kujali matokeo ya uchaguzi wa urais.
"Lakini inapaswa kujulikana kuwa tuna matumaini makubwa kwamba matokeo yanatupendelea."