In Summary

• Johnson Sakaja aliapishwa kama gavana wa nne wa Nairobi.

• Sakaja alimshinda Igathe na kuzoa kura 699, 392 huku Igathe akipata kura 573, 516.

JOHNSON SAKAJA Johnson Sakaja akiwa na mkewe wakati wa kuapishwa kwake kama Gavana wa Nairobi mnamo Agosti 25, 2022.
Image: EZEKIEL AMINGA

 Johnson Arthur Sakaja sasa ndiye rasmi Gavana mpya wa Nairobi. Aliapishwa katika hafla rasmi iliyofanyika KICC.

Jaji Roselyne Aburili kwa kusaidiwa na hakimu Caroline Kabucho waliwaapisha Sakaja na naibu wake, Njoroge Muchiri.

Mbali na hayo, hakimu pia anasimamia utiaji saini wa hati ya uadilifu kwa wawili hao.

Akizungumza baada ya kuapishwa kwake Sakaja alifichua ni kwa nini mpinzani wake Polycarp Igathe alikosekana kwenye hafla hiyo.

"Nataka kumtambua mshindani wangu Igathe. Nilikaa naye hivi majuzi na alijipa udhuru leo ​​akisema anasafiri. Kugombea madaraka ni kitendo cha uzalendo. Asante Polycarp kwa kusogeza mbele siasa zetu kwa njia chanya zaidi. Wewe ni mfano halisi wa Siasa safi, kitu ambacho ninaamini."

Sakaja aliwashukuru wagombea wengine wote wa ugavana akiongeza kuwa anatumai wanaweza kufanya kazi pamoja.

Alisema alifurahi kuwa kampeni ya 2022 haikuegemea utambulisho wa kibinafsi bali ajenda zinazowaunganisha Wakenya. Aliwashukuru wenyeji wa Nairobi kwa kudumisha amani.

Sakaja hivi majuzi alikutana na Igathe kwa tafrija ya kahawa jambo lililowafanya Wakenya kushangaa. Wengi walidhani ni maadui kutokana na kuwa wanawania kiti kimoja lakini hiyo ni mbali na ukweli.

View Comments