logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Wachaneni na maisha ya watu,'Sonko awashambulia wanaomkejeli mkewe Guardian Angel

Esther Musila alipokea kejeli nyingi kwa sababu amemuacha msanii huo zaidi ya miaka 20.

image
na Radio Jambo

Habari26 May 2021 - 10:21

Muhtasari


  • Sonko awashambulia wanao mkejeli mkewe Guardian Angel

Msanii wa nyimbo za injili Guardian Angel alimvisha mpenzi wake pete ya uchuba JUmanne huku akisheherekea siku yake ya kuzaliwa.

Esther Musila alipokea kejeli nyingi kwa sababu amemuacha msanii huo zaidi ya miaka 20.

Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko amegadhabishwa na kejeli za wanamitandao, na kutetea uhusiano kati ya Guardian Angel na Esther Musila.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa facebook Sonko alisema kwamba watu wanapaswa kuachana na maisha ya wengine kama wanataka kuendelea.

"Mrembo huyu anaitwa Esther Musila anafanya kazi na UN ... ana miaka 51 .... jana alichumbiwa na mwanamuziki wa injili Guardian Angel wa miaka 30

Nimeona tu watu wenye nia mbaya wakimtia maneno mabaya kama bibi yake. Hii sio haki kabisa

Nyinyi mukitaka pia muowane ama muolewe wachaneni na maisha ya watu. Buree kabisa nyinyi

wewe Esher na Guardian Angel Hongera kwa ndoa yako, ninawatakia maisha ya Upendo na furaha. Miaka ijayo na ijazwe na furaha ya kudumu." Aliandika Sonko.

Licha ya kejeli nyingi kutoka kwa mashabiki wawili hao wamezidi kuonyesha kuwa 'Age is just a number' bali mapenzi ya kweli yanadumu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved