logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ringtone aapa kumfichua Guardian Angel hadharani

Ringtone alisema kuwa Guardian Angel ni mnafiki na kuna mambo anayofanya ambayo atafichua siku ya Alhamisi.

image
na Radio Jambo

Burudani26 May 2021 - 20:24

Muhtasari


•Alisema  kuwa atahutubia wanahabari kuhusu vitu fiche ambazo  Guardian Angel anafanya

•Ringtone alimtaja Guardian Angel kuwa mnafiki

Ringtone Apoko

Mwanamuziki wa nyimbo za injili mwenye utata mwingi, Ringtone Apoko amemkashifu mwanamuziki mwenzake, Guardian Angel huku akimuita Mkristiano bandia.

Kupitia mtandao wa Instagram, Apoko ameapa kutoa ujumbe kwa wanahabari akimfichua Guardian Angel.

"Kesho naenda kumfichua Guardian Angel vibaya sana na nafikiria sasa ananenda kuisha. Kuna vitu amefanya na anajifanya bado, namfichua kesho" Ringtone alitangaza.

Mwanamuziki huyo ambaye anajitambulisha kama mwenyekiti wa wanamuziki wa nyimbo za injili amewaagiza Wakenya kusubiri uvumbuzi mkubwa kumhusu Guardian Angel.

"Kesho saa nne naita wanahabari, tayarisheni simu zenu, tafuteni wakati, ombeni ruhusa kutoka kazini kwani namfichua Guardian Angel na sina mchezo" Alidai Ringtone.

Msanii Guardian Angel alitoa ombi la ndoa kwa mpenzi wake, Esther Musila ambaye alisema NDIO. Tusubiri ujumbe wa Ringtone tuskie ana yepi ya kusema kumhusu Guardian Angel...


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved