logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vanessa Mdee na mwigizaji Rotimi waandika kitabu cha Kiswahili

Vanessa alisema kuwa amekuwa akitia bidii sana kumfunza Kiswahili mpenzi wake , Rotimi mzaliwa wa Marekani , kwani hiyo ndiyo lugha yake ya mama

image
na Radio Jambo

Burudani27 May 2021 - 05:55

Muhtasari


•“Katika safari yangu ya  kusoma Kiswahili, nataka nitembee nanyi. Mimi na mke wangu tumeandika kitabu cha Kiswahili kwa jina Swahili 101” Alisema Rotimi.

Vanessa Mdee na Rotimi

Mwanamuziki mashuhuri toka Bongo, Vanessa Mdee ameshirikianak na mpenzi wake ambaye ni mwigizaji Olurotimi Akinosho almaarufu kama Rotimi kuandika kitabu cha Kiswahili kwa jina Swahili 101.

Wakizindua kitabu hicho kwenye mtandao wa Instagram, Rotimi ambaye ni mzaliwa wa Marekani kwa wazazi kutoka Nigeria amesema kuwa uandishi wa kitabu hicho ni moja kati ya hatua walizochukua ili ajue kuzungumza Kiswahili.

“Katika safari yangu ya  kusoma Kiswahili, nataka nitembee nanyi. Mimi na mke wangu tumeandika kitabu cha Kiswahili kwa jina Swahili 101” Alisema Rotimi.

Vanessa alisema kuwa amekuwa akitia bidii sana kumfunza Rotimi Kiswahili kwani hiyo ndiyo lugha yake ya mama.

“Kama mnavyojua kuwa mimi nazungumza lugha tatu Kiswahili ikiwa lugha yangu ya mama, tumejifunza kutokana na uzoefu kuwa njia rahisi sana na inayofanya kazi katika kujifunza lugha ni kuitumia katika harakati zote za kila siku maishani” Mdee alisema.

Wawili hao walitaja haswa kupenda sana maneno kama ‘Asante’, ‘Nakupenda’ na ‘Mama Yangu’.

Rotimi aliagiza mashabiki wake kununua kitabu hicho kwani hio ni njia ya kusaidia bara Afrika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved