logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rapa Noti Flow hatimaye ajitambulisha kuwa shoga

Noti Flow hapo zamani alikuwa kwenye uhusiano na rapa mwenzake Kanali Mustapha

image
na Radio Jambo

Habari31 May 2021 - 11:35

Muhtasari


  • Rapa Noti Flow ameonyesha rasmi kuwa yuko kwenye uhusiano na rafiki wa kike, anayejulikana kama Mfalme Alami

Rapa Noti Flow ameonyesha rasmi kuwa yuko kwenye uhusiano na rafiki wa kike, anayejulikana kama Mfalme Alami.

KUpitia kwenye ukurasa wake wa instagram, Noti Flow alishiriki tena video na King Alami huku mashabiki wakisifia mapenzi yao, na kuonekana wakiwa kwenye mahabara  ya mapenzi kweli kweli.

Mapema mwezi wa Mei, uhusiano wa rapa huyo na King Alami ulitoa uvumi kwamba walikuwa wakichumbiana kwani wote walionekana wazuri pamoja.

"Usiku wetu wa kwanza kutengana tangu tuhamie pamoja na ninaamka kwa hii 🥺😭😭😭😭 Ananippeda kama vile nampenda 💘 Hakuna mtu anayepaswa kutenganisha  aina hii ya mapenzi ❤️❤️❤️❤️❤️❤️❤️❤️🦄️ 🦄 🌈 ," Aliandika Noti Flow.

KUpitia kwenye picha nyingine aliopakia wakiwa wawili Noti flow aliandika ujumbe  unaodhitibitisha kuwa ni shoga  katika ujumbe huo alisema haya.

"Kila kitu nilichokuwa nikitaka ndani yake nimepata kwake ❤️."

Noti Flow hapo zamani alikuwa kwenye uhusiano na rapa mwenzake Kanali Mustapha lakini wawili hao wakaachana.

Noti Flow kwa upande wake alisimulia kuwa aliamua kutia kikomo kwa uhusiano huo kutokana na Mustafa kukosa kuwa na malengo mwafaka kwa maisha .

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved