logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Yeye ni nani, amewafanyia nini?" Akothee akiri kutomjua Embarambamba

Akothee alisema kuwa Wakenya wana mazoea sana ya kumtumia yeyote aliyewakosea.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri31 May 2021 - 03:28

Muhtasari


•Shabiki mmoja alitengeneza chapisho la kumtania Akothee kuwa aliwanga anajitayarisha kupatana na Embarambamba

•Akothee alisema kuwa alikuja kuskia kuhusu Embarambamba kutokana na jumbe za mashabiki kwenye ukurasa wake.

Akothee akifanya tizi

Mwanamuziki na mwanabiashara mashuhuri, Esther Akoth amekiri kuwa amekuja kumsikia Embarambamba kutokana na jumbe za mashabiki kwenye ukurasa wake.

Akothee amesema kuwa huwa hatazami runinga na kuwataka mashabiki kumuelezea Embarambamba ni nani.

"Nimekuja kuskia kuhusu Embarambamba kupitia jumbe mnazoandika hapa. Yeye ni nani? mnisamehe huwa sitazami runinga. Ningetaka kujua yeye ni nani haswa na amefanya nini? Akothee aliuliza kupitia mtandao wa Instagram.

Hii ni baada ya shabiki mmoja kutengeneza chapisho la kumtania Akothee amaarufu kama 'memes' akisema kuwa Akothee anajitayarisha kumwona Embarambamba.

Mwanzilishi huyo wa Akothee safaris alisema kuwa Wakenya wana mazoea ya kumtumia kila aliyewakosea.

"Najua kila mwenye amewakosea Wakenya huwa natumiwa Akothee. Embarambamba amewafanya nini" Akothee alitaka kujua.

Embarambama amekuwa akienea mitandaoni kwa muda kutokana na sarakasi nyingi anazofanya kwa nyimbo zake na drama zinazomkumba. Wiki iliyopita video mbili zilisambazwa mitandaoni ambapo alionekana akishirika kwenye densi isiyo ya kimaadali na mashabiki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved