logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Amekuwa akinitunza kama yai" Vera asema kuwa mumewe amekuwa akimtumikia

Mwanasoshalaiti huyo amefichua kuwa amekuwa kwenye mahusiano  mengi mabaya hapo awali, mengine tusiyoyajua

image
na Radio Jambo

Yanayojiri17 June 2021 - 07:24

Muhtasari


•Bae ndiye binadamu wa ajabu zaidi. Haswa  zaidi tangu tugundue kuwa tutakuwa na mtoto hivi karibuni. Katika safari yangu ya ujauzito, amekiuka na kunitunza kama yai. Sigusi chochote, anahakikisha kuwa nakula matunda kila siku. Ananilisha  cha lazima, ananipikia na anasugua miguu yangu” Vera alisema

Vera Sidika na Brown Mauzo

Mwasoshalaiti Vera Sidika amemsifu mpenzi wake Brown Mauzo kwa kumtumikia wakati wa ujauzito wake.

Vera amethibitisha kuwa hajakuwa akifanya kazi yoyote pale nyumbani kwani mumewe amekuwa akimtunza kama yai.

Bae ndiye binadamu wa ajabu zaidi. Haswa  zaidi tangu tugundue kuwa tutakuwa na mtoto hivi karibuni. Katika safari yangu ya ujauzito, amekiuka na kunitunza kama yai. Sigusi chochote, anahakikisha kuwa nakula matunda kila siku. Ananilisha  cha lazima, ananipikia na anasugua miguu yangu” Vera alisema

Mwanasoshalaiti huyo ambaye alipata umaarufu mkubwa kufuatia kuhusishwa kwa wimbo wa P Unit, ‘You Guy’ , ameshukuru Mungu kwa kumpa bwana mzuri hata baada ya kupitia kwenye mahusiano mabaya.

Kweli Mungu alijionyesha wakati alikuleta maishani mwangu. Nimekuwa kwenye mahusiano mabaya zaidi, mengine hamukuyajua. Ila hayo hayakunizuia kupenda tena” Vera aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Ameapa kuwa hatawahi sita kumpenda mwanamuziki Brown Mauzo.

Hapo awali, Vera amechumbia takriban watu watatu wanaojulikana wakiwemo mwanamuziki Otile Brown, daktari Mtanzania Jimmy Chansa na Yommy Johnson kutoka Nigeria

Jioni ya Jumatano, Vera alisisimua mitandao baada ya kufichua kuwa alikuwa mjamzito. Hata hivyo, hakubainisha jinsia ya mtoto wake .

Ametangaza kuwa bado hajatambua jinsia huku akisema kuwa amekuwa akisubiria sana kujua.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved