logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nitangoja sheria ichukue mkondo wake,niombeeni,'Ringtone azungumza

Mwimbaji huyo anaonekana na bandeji kwenye uso na pia mkono wake wa kulia

image
na Radio Jambo

Habari24 July 2021 - 07:09

Muhtasari


  • Hatimaye msanii Ringtone azungumza baada ya kuchapwa
  • Kupitia kwenye Instagram alishiriki video ambapo, Apoko amewashukuru mashabiki wake na madaktari kwa kumtakia afya njema.

ringtone apoko

Mwimbaji mashuhuri Ringtone Apoko amezungumza kwa mara ya kwanza tangu kugombana kwake na mwanablogu Robert Alai.

Kupitia kwenye Instagram alishiriki video ambapo, Apoko amewashukuru mashabiki wake na madaktari kwa kumtakia afya njema.

Alifichua kwamba alikuwa ametoka nje ya hospitali ya Kenyatta ambapo alitibiwa baada ya kuchukua p3.

"Nataka kuwashukuru Wakenya wote ambao waliniombea baada ya shambulio na pia nataka kuwashukuru madaktari wa hospitali ya Kenyatta ambao walinitibu Nataka tu mashabiki waendelee kuniombea, "alisema.

Pia amesema ataendelea kuchukua dawa na kifichua kwamba ataziruhusu sheria ziamue kati ya makabiliano yake na Robert Alai.

Mwimbaji huyo anaonekana na bandeji kwenye uso na pia mkono wake wa kulia unaonekana kuumizwa kama matokeo ya ugomvi.

"Nitangoja sheria ichukue mkondo wake,"

Vita vyao vilitokea siku ya Ijumaa, ambapo ilisababisha mwanablogu Alai kukamatwa kwa madai ya kumshambulia msanii huyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved