logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Nina bahati kuwa nawe kando yangu" Zari aandikiwa ujumbe maalum na mpenziwe akiadhimisha kufikisha miaka 41

'The Dark Stallion' alimtambulisha mama huyo wa watoto watano kama mkewe na kudai kwamba anajivunia sana kuhusiana naye.

image
na Radio Jambo

Burudani24 September 2021 - 04:56

Muhtasari


•Uhusiano kati ya wawili hao umeonekana kama kwamba ulizama tangu mwezi Julai wakati Zari alifuta picha za raia huyo wa Nigeria kwenye ukurasa wake wa Instagram.

•Siku ya Alhamisi @lyamzey_don alimwandikia Zari ujjumbe wa kipekee alipokuwa anasherehekea kufikisha miaka 41.

•'The Dark Stallion' alimtambulisha mama huyo wa watoto watano kama mkewe na kudai kwamba anajivunia sana kuhusiana naye.

Huenda mwanasoshalaiti mashuhuri  kutoka Uganda Zari Hassan hajatengana kabisa lucky in na mpenzi wake 'The Dark Stallion' kama ilivyodhaniwa na wengi.

Uhusiano kati ya wawili hao umeonekana kama kwamba ulizama tangu mwezi Julai wakati Zari alifuta picha za raia huyo wa Nigeria kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Hata hivyo, huenda bado mapenzi yamenoga kati yao kama chapisho la Stallion la hivi karibu kwenye mtandao wa Instagram linavyoashiria.

Siku ya Alhamisi @lyamzey_don alimwandikia Zari ujjumbe wa kipekee alipokuwa anasherehekea kufikisha miaka 41.

'The Dark Stallion' alimtambulisha mama huyo wa watoto watano kama mkewe na kudai kwamba anajivunia sana kuhusiana naye.

"Kheri za kuzaliwa kwa mwanamke anayeleta mwangaza maishani mwangu. Mpenzi wangu anayejali na mke nimpendaye. Wewe ndiye naweza ambia siri zangu na nina bahati sana kuwa nawe kando yangu. Kuwa na siku njema ambayo unastahili mke wangu mrembo. Kheri za kuzaliwa mama Pinto" Aliandika Stallion.

Miezi miwili iliyopita Zari matendo ya Zari kwenye mtandao wa Instagram yaliibua dhana kwamba kitumbua kilikuwa kimeingia mchanga na wawili hao walikuwa wamemua kukatiza uhusiano wao.

"Nampeza lakini ilibidi nimuache aende. Kama halinijengi basi sitaliweka" aliyekuwa mpenzi wa Diamond Platnumza aliandika, ujumbe ambao ulionekana kuzungumzia Stallion.

Kabla ya hayo Zari alikuwa na mazoea ya kupakia picha zao kwenye ukurasa wake ila baada ya hapo hajaonekana tena akizipakia. The Stallion hata hivyo amepakia picha kadhaa baada ya hapo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved