logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Ni kama nitakufa" Ringtone adai kuwa aliathirika vibaya baada ya kupigwa rungu na Robert Alai

Ringtone amedai kwamba anapanga kuenda hospitalini kufanyiwa upasuaji kwani amekuwa akiumwa sana na kichwa hadi anakosa usingizi.

image
na Radio Jambo

Habari06 October 2021 - 09:05

Muhtasari


•Ringtone amedai kwamba anapanga kuenda hospitalini kufanyiwa upasuaji kwani amekuwa akiumwa sana na kichwa hadi anakosa usingizi.

Mwanamuziki Alex Apoko amesihi mashabiki wake kumkumbuka kwa maombi akidai kuwa amekabiliwa na maumivu mabaya kichwani kufuatia vita kati yake na mwanablogu Robert Alai takriban miezi miwili iliyopita.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ringtone amedai kwamba aliathirika vibaya baada ya kugongwa kwa rungu kichwani na Alai mwezi Julai.

Ringtone amedai kwamba anapanga kuenda hospitalini kufanyiwa upasuaji kwani amekuwa akiumwa sana na kichwa hadi anakosa usingizi.

"Najaribu kufanya mazoezi. Kichwa kinauma,sijalala.Ile rungu niligongwa hapa iliniathiri. Nataka kuenda kufanyiwa upasuaji. Mniombee, sioni kama nitaponea, ni kama nitakufa. Niombeeni" Ringtone alisema.

Hata hivyo msanii huyo wa nyimbo za injili ameeleza matumaini yake kuwa Mungu atamponya  huku akidai kwamba iwapo atafariki, mwanablogu aliyempiga rungu ndiye atakuwa amesababisha kifo chake.

Miezi miwili iliyopika msanii huyo alidai kuwa alienda hadi Afrika Kusini kupokea matibabu maalum kufuatia mvurugano ambao ulifanyika katika barabara moja jijini Nairobi.

Mwanamuziki huyo ambaye anajitambulisha kama mwenyekiti wa  muungano wa wanamuziki wa nyimbo za injili alimshtaki Alai kwa kusababisha madhara mwilini wake na kuvunja kioo cha gari yake aina ya Range Rover wakati walikuwa wanazozana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved