logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilipoteza fahamu kwa siku nne-Akuku Danger azungumza

Alilazwa kwa takriban miezi miwili katika Hospitali ya Nairobi West na alitoa shukrani kwa marafiki

image
na Radio Jambo

Burudani16 February 2022 - 09:15

Muhtasari


  • Mchekeshaji huyo alifichua kuwa aliambiwa mapafu yake yanashida na pia alikuwa ameshikwa na homa ya mapafu katika mchakato huo
Magonjwa yaliyokuwa yameshambulia Akuku Danger yafichuliwa

Mcheshi Akuku Danger amezungumza kuhusu ugonjwa uliomfanya alazwe hospitalini kwa zaidi ya mwezi mmoja.

Akuku Danger alizaliwa na Sickle Cell Anemia, alipata matatizo ya kifua mnamo Desemba, na kusababisha kulazwa katika Hospitali ya Nairobi West.

"Ninaujua mwili wangu na kwa kuwa nimekuwa na anemia ya sickle cell tangu kuzaliwa, najua kunapotokea tatizo. Nilipojipeleka hospitalini nilikuwa na matatizo ya kupumua

Nililazwa mara moja na baadaye nilihamishiwa Nairobi West Hospital ICU ambapo nilipoteza fahamu kwa siku nne,"," Akuku aliambia Standard.

Mchekeshaji huyo alifichua kuwa aliambiwa mapafu yake yanashida na pia alikuwa ameshikwa na homa ya mapafu katika mchakato huo.

Alilazwa kwa takriban miezi miwili katika Hospitali ya Nairobi West na alitoa shukrani kwa marafiki, familia na watu wema waliosaidia kulipia bili kubwa ya matibabu.

“Kupitia paybill tulifanikiwa kukusanya karibu Sh3milioni ambazo zililipa bili yangu ya kwanza ya matibabu. Msaada ulikuwa mwingi

Kwa sasa nina salio la Sh1.3milioni ambalo ninapaswa kufuta katika siku 60 zijazo," alisema, na kutoa wito kwa umma kusaidia kwa njia yoyote iwezekanavyo.

Mnamo Februari 8, Akuku Danger aliondolewa kwenye kituo hicho baada ya kulipa bili ya karibu Sh 3 Milioni.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved