logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nameless aorodhesha mambo atakayo mfanyia Wahu anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa

Kupitia kwenye ujumbe wake alimshukuru mkewe kwa kuwa naye maishani, na kumfanya kuwa mtu bora.

image
na Radio Jambo

Makala22 March 2022 - 08:33

Muhtasari


  • Kupitia kwenye ujumbe wake alimshukuru mkewe kwa kuwa naye maishani, na kumfanya kuwa mtu bora.

Huku msanii Wahu Kagwi akisherehekea siku yake ya kuzaliwa, mumewe Nameless kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram ameorodhesha mambo ambayo atamfanyia siku hii maalum.

Kupitia kwenye ujumbe wake alimshukuru mkewe kwa kuwa naye maishani, na kumfanya kuwa mtu bora.

Wawili hao wameonyesha mfano mwema kwa wanandoa, huku wakiwa kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 10.

Moja wapo ya mambo ambayo msanii huyo aliorodhesha ni kwamba atakuwa dereva wa mkewe kwa siku, atampikia na chochote kile atataka.

Huu hapa ujumbe wake;

"Birthday Gal♥️♥️♥️MamaTumiso🧐... Obviously Today anything unasema kwa nyumba is the law... Tunajua🙄🤪...ni utamaduni wa Mathenge, take advantage...ni leo tu.😊. Fam nisaidieni kumtakia rafiki yangu heri njema siku yake ya kuazaliwa. wewe ni baraka katika maisha yangu.. Character development umenipatia weuh 😅😅😅...mimi ni mtu bora kwa ajili yako😁... HAPPY BIRTHDAY babe...

I am at your service, I will be your Uber driver, cook ,masseuse, boy toy, mubaba chochote unataka😅😅 .. uliza utapewa, lakini ni ya Leo tu🧐. #ReadyToServe," Nameless Aliandika.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved