logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Iliniuma-Otile Brown ataja sababu ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Nabii

Otile Brown alisema kuwa haikuepukika kwa sababu ya masuala kadhaa ambayo yanaeleweka.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri07 June 2022 - 08:20

Muhtasari


  • Otile Brown ataja sababu ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Nabii

Tangu kuachana na Nabii, Otile Brown amekuwa kimya sana na tumekuwa tukimuona peke yake, akiachia nyimbo na kutofanya mahojiano yoyote na wanablogu au hata Vituo vya Tv miezi 6 iliyopita.

Mtangazaji Ali alipata nafasi ya kufanya mahojiano na Otile Brown na akamuuliza kuhusu kuachana kwake na Nabii.

Otile Brown alisema kuwa haikuepukika kwa sababu ya masuala kadhaa ambayo yanaeleweka.

Jambo la kwanza, Nabii hakuwa tayari kuhamia Kenya kwa sababu ya baadhi ya masuala ya kifamilia ambayo yalikuwa muhimu sana katika tamaduni za Waethiopia, jambo lingine lilikuwa ni kuhusu baadhi ya mambo ambayo yalitaka awe nje ya Kenya.

Uhusiano wa umbali mrefu haukufaulu na kwa sababu zisizoweza kuepukika wakati mwingine Nabii angeweza kuchukua muda mrefu sana kurejea Kenya.

Otile alisema kuwa wote wawili walikubali na kuamua kuachana, na labda ikiwa imepangwa wao kuoana, inaweza kutokea siku zijazo.

Huku akizungumzia ugomvi wake na  Arrow Bwoy miezi michache iliyopita, Otile alisema kuwa Arrow alitoa kolabo hiyo bila ridhaa yake - akielezea hatua hiyo kama isiyojali na isiyo ya kitaalamu.

"Tulikuwa tumezungumza na Arrow Bwoy ni miongoni mwa wasanii niliowaheshimu sana. Ninawaheshimu nyote na ninamuogopa Mungu sana," Otile alisema.

"Arrow Bwoy aliniuliza kama tunaweza kutoa wimbo huo na nikasema hatuwezi kuutoa kwa vile wimbo huo ulikuwa wa zamani lakini akaendelea na kuutoa."

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved