logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Museveni amwandikia mkewe ujumbe wa kipekee anapoadhimiasha miaka 74

Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni ameandika ujumbe mtamu kwa mkewe

image
na Radio Jambo

Yanayojiri24 June 2022 - 09:37

Muhtasari


  • Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni ameandika ujumbe mtamu kwa mkewe anapofikisha umri wa miaka 74 leo
  • Museveni pia alifichua kuwa Mama Janet amejitolea kwa Mungu, familia ya Museveni na watu wote wa Uganda

Ni nadra sana kwa wakati huu wa sasa wanandoa kudumu kwenye ndoa zao hadi,wazeeke au kifo kitakapowatenganisha.

Swali kuu ambalo linasalia akilini mwa watu wengi, sababu kuu ya ndoa za karne hii ya sasa kuvunjika kila kuchao ni ipi?

Kusherehekea siku yako ya kuzaliwa kila mwaka ukiwa na afya njema, na uko mzima ni moja wapo ya zawadi kuu ambayo kila mmoja anapaswa kumshukuru Mungu Kwalo.

Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni ameandika ujumbe mtamu kwa mkewe anapofikisha umri wa miaka 74 leo.

Kupitia akaunti yake rasmi ya twitter, Museveni alimpongeza Mama Janet huku akimtakia miaka mingi zaidi ya afya njema, mafanikio na furaha.

Museveni pia alifichua kuwa Mama Janet amejitolea kwa Mungu, familia ya Museveni na watu wote wa Uganda.

"Nampongeza sana Maama Janet kwa kufikisha umri wa miaka 74, namshukuru Mungu kwa uhai wake, asante Janet kwa upendo na kujitolea kwako kwa Mungu, familia yetu na wananchi wa Uganda, akupe miaka mingi zaidi ya afya njem,"Museveni aliandika.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved