logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mimi si mjamzito-Wema Sepetu asema

Wema Sepetu alidai kuwa hata angalikuwa mjamzito, hawezi kuitangazia kwa watu.

image
na

Yanayojiri17 March 2023 - 07:45

Muhtasari


• Sepetu alidokeza kuwa hajakata tamaa kupata mtoto.

• Alieleza pia kuwa angependa kupata mtoto wa kiume.

Muigizaji mashuhuri nchini Tanzania Wema Sepetu amekanusha madai ya kuwa na mimba.

Mwanamitindo huyo alisema kwamba hata kama angekuwa mjamzito  hangetangazia dunia.

"Sina mimba. Hata nikipata mimba, unadhani nitalizungumzia? Kama vile Mungu anaposema, 'Nibariki tumbo lako' kisha nipate mimba, sitakuambia. Lakini natamani kuwa mjamzito tuseme Inshallah", aliandika kwenye Instastories.

Aliongeza kuwa alihitaji mtoto wa kiume. "Na hapo itakuwa bora zaidi ikiwa ni mtoto wa kiume anayefanana na mama yake."

Mwaka jana, Sepetu na mpenzi wake Whozu walifichua kwamba alipata mimba.

“Wema alikuwa mjamzito mwezi Agosti, ilipofika takribani miezi mitatu tuligombana na nusura tuachane, mimi ndiye niliyekuwa kwenye makosa na nilimkasirikia Wema na kushindwa kumsikiliza, nilitamani kuachana naye tu." Whozu alieleza.

"Sikujua kwamba hiyo ingeathiri ujauzito. Sikuwa muungwana, nampenda na nilihisi ameniumiza." Aliongeza.

"Aliomba nimsamehe na sikuweza kusikiliza. Nilipewa taarifa kwamba alikuwa ametoa mimba...Ananitumia ujumbe akisema 'Hicho ndicho ulichotaka, una furaha?' Nilihisi kuchanganyikiwa na alilia sana." "Nilijiuliza maswali mengi. Nilijuta."

Kwa upande mwingine Sepetu alidokeza kuwa hajakata tamaa ya kutafuta mtoto. Aliongeza kuwa madaktari walimshauri kujiepusha na msongo wa mawazo na kupumzika.

“Tunapogombana inakaa kati yetu na hatupendi kuiweka hadharani, sitaki kuwashirikisha watu katika mambo mengi yanayotokea katika maisha yetu, tunapenda kuona watu wanatuona tunapendana. Mengine lakini tuwekee matatizo sisi wenyewe."

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved