logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mambo yamechemka: Carol Katrue mpenzi wa Miracle Baby atangaza yuko 'single'

Wenzi hao walimkaribisha mtoto wao wa kwanza pamoja Februari, 18 2023.

image
na Davis Ojiambo

Burudani31 March 2023 - 08:56

Muhtasari


  • • Miracle Baby hata hivyo ana watoto wengine wanne na wanawake tofauti.
  • • Katika mahojiano ya awali, msanii huyo aliwahi nukuliwa akisema kwamba ndoto yake ni kuwa na watoto 17.
Carol Katrue atangaza kuwa singo

Carol Katrue, mpenzi wa msanii wa gengetone Miracle Baby ametangaza kuwa yuko singo, siku chache tu baada ya kudokeza kuwa na mimba ya pili.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Katrue aliandika maneno “niko single” na kuweka emoji za kulia, pasi na kutoa taarifa Zaidi kuhusu kilichojiri.

Haijulikani kama ni kiki ya mitandaoni anatafuta au ni kweli wameachana na Miracle Baby.

Hii inajiri wiki mbili tu baada ya Katrue kutangaza kwamba alikuwa na ujauzito wa pili tena, mwezi mmoja tu baada ya kujifungua mtoto.

Carol Katrue aliingia kwenye mitandao ya kijamii Jumamosi 18 na kutangaza habari hiyo, akichapisha kifaa cha kupima ujauzito kwenye hadithi zake za Instagram na nukuu: "Kuna moto mlimani."

Mpenzi wake Miracle Baby, kwa upande wake, aliweka kifaa hicho cha ujauzito na kuandika: “...ni wiki tatu tangu kuzaliwa kwa mtoto hii nayo imejitokeza,” akiendelea na kuongeza; "beb samahani."

Katrue ambaye pia ni msanii walikutana na Miracle Baby miaka michache iliyopita baada ya mambo kumwendea mrama Miracle Baby katika kundi la Sailors Gang ambao walikuwa wanatamba na vibao moto vya gengetone.

Miracle Baby na Katrue walishikana pamoja na kuanza kuimba nyimbo za Mugithi, ambapo wamejizolea ufanisi mkubwa, mbali na gengetone.

Wenzi hao walimkaribisha mtoto wao wa kwanza pamoja Februari, 18 2023. Miracle Baby hata hivyo ana watoto wengine wanne na wanawake tofauti.

Katika mahojiano yaliyopita, alisema: “Mmoja aliachwa mlangoni kwangu kwenye beseni kwa hivyo ilinibidi kumlea. Hata hivyo, tunafanana na ninashuku kuwa yeye ni wangu.”

Alipoulizwa kwa nini hawezi kutulia na mwanamke mmoja, alisema anataka kuwa na watoto 17 katika maisha yake na hakuna mwanamke mmoja anayeweza kukubali kuzaa na kuwalea wote.

"Hakuna mwanamke atakayekubali kuzaa watoto 17. Mama wa watoto wanajuana na wako kwenye mahusiano mazuri," alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved